Quantcast
Channel: MC DR CHENI
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2428

Mastaa wa Bongo Movies Mashabiki wa Yanga Wafungua Tawi la Yanga

$
0
0
MASTAA wa Bongo Movies wanaoshabikia Timu ya Yanga wamefungua tawi rasmi kwa ajili ya kuisapoti hiyo ya Jangwani.
MIKE
Mike Sangu akiwa na Esha Buheti
Yanga imekuwa na mashabiki wengi kila kona hapa nchini na Bongo Movies wameanzisha tawi hilo ili kuwa karibu zaidi na timu hiyo.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tawi hilo, Mike Sangu, baada ya kuona wanajitosheleza kufungua tawi lao waliamua kukutana na kuhimizana kufungua tawi pamoja na kuchagua viongozi mbalimbali.
“Tulipokubaliana tuliongea na Jerry Muro (ofisa habari wa Yanga) ambaye alitusaidia kupata usajili na sasa tunatambulika rasmi,” alisema Mike.
Aliwataja wasanii wengine wanaounda tawi hilo ambao wote ni wachezaji filamu kuwa ni, Wema Sepetu, Baby Madaha, Isabela Mpanda, Miriam Jolwa ‘Kabula’, Halima Yahaya ‘Davina’, Esha Buheti, Flora Mvungi, Jimmy Mafufu, Jack Pentizel, Mayasa Mrisho, Catherine Ambakisye ‘Mama Rolaa’, Sauda Mwilima, Hassan Moshi, Sabrina Rupia ‘Cathy’, Mary Mawigi, Vincent Kigosi ‘Ray’ na wengine wengi.

Chanzo: GPL

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2428

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>