Quantcast
Channel: MC DR CHENI
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2428

MSANII BARNABA AKATAA KAZI ZA KISHIKAJI KWENYE STUDIO YAKE

$
0
0
Msanii wa bongo fleva Barnaba ambaye pia ni mmiliki wa studio za high table sound amefunguka na kusema kuwa hataki kufanya kazi ‘kishikaji’ kwenye studio yake.

Barnaba ameweka wazi kuwa studio nyingi zinakufa kwa sababu watu wanafanya kazi kijamaa lakini kwa upande wake amesema kuwa lazima afanye kazi zenye faida hata kama mtu hana hela na anataka kurekodi lazima wao waaangalie watanufaika vipi kwenye huo wimbo baada ya kutoka ikiwemo kwenye mauzo ya mitandaoni,ring back tone,endorsement na kadhalika.
Kwenye studio yangu tunachaji bei ambayo sio ya kutisha saana chochote tunaweza kupokea kutegemea vile tunavyoongea lakini ushikaji sina na sitaki kabisa kwenye studio yangu,Mimi huwa nathamini kwanza kipaji cha mtu hata kama mtu huna hela kuna namna tunaongea kuhusu benefits lakini sio mambo ya kishikaji shikaji” alifunguka Baranaba ambaye alidai lengo kubwa la studio hio ni kuuweka muziki wa bongo kwenye ramani nzuri.
Souce: HZB TV

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2428

Trending Articles