‘Karibu Kiumeni’ haitarajiwi tu kuja kuwa filamu ya Bongo yenye mafanikio zaidi kuwahi kutokea, bali pia itakuwa filamu ya kwanza iliyokutanisha mastaa wengi zaidi wa Bongo Flava kurekodi original soundtrack yake.
![14515676_717016541780719_8093899339992137728_n](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2016/10/x14515676_717016541780719_8093899339992137728_n.jpg.pagespeed.ic.Y1gd0fNvUy.jpg)
P-Funk Majani ndiye mtayarishaji mkuu wa soundtrack ya filamu hiyo inayotarajiwa kutoka December mwaka huu. Soundtrack itajumuisha orodha ndefu ya mastaa wa Bongo Flava
Karibu Kiume ni filamu iliyochezwa na Ernest Napoleon (Going Bongo), Irene Paul, Idris Sultan na mastaa wengine na inatarajiwa kutoka December mwaka huu.
Napoleon ameshare picha Instagram akiwa na waimbaji nguli wa Bongo Flava watakaorekodi soundtrack hiyo inayosimamiwa na P-Funk Majani wa Bongo Records.
![14488313_1814478955461842_7566158987297554432_n](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2016/10/x14488313_1814478955461842_7566158987297554432_n.jpg.pagespeed.ic.RGiD4_SR2I.jpg)
Kutoka Kushoto: Inspekta Haroun, Adili, Ernest Napoleon, Juma Nature na P-Funk aliyekatwa
“#kiumenimovie all star soundtrack by #pfunkmajani loading #jumanature #inspektaharun #tid #youngkiller #dogojanja #adili #msagasumu #damiansoul,” ameandika Napoleon kwenye picha hiyo.
Wasanii watakaosikika ni pamoja na TID, Inspekta Haroun, Juma Nature, Adili, Young Killer, Msagasumu, Damian Soul na Adili.
![14504839_1704131339914051_3020845503676940288_n](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2016/10/x14504839_1704131339914051_3020845503676940288_n.jpg.pagespeed.ic.dqblEU7f8x.jpg)
Napoleon akieleza jambo. Pembeni yake ni Juma Nature
![14540419_1816035215308570_2201581797634998272_n](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2016/10/x14540419_1816035215308570_2201581797634998272_n.jpg.pagespeed.ic.3OfnFhVQJK.jpg)
Crew nzima itakayohusika kupika soundtrack ya Karibu Kiumeni ikiwa nje ya studio za Bongo Records jijini Dar es Salaam
![14549895_1582917945351423_2561635855315763200_n](http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2016/10/x14549895_1582917945351423_2561635855315763200_n.jpg.pagespeed.ic.NHmq37BJvP.jpg)
Kutoka Kushoto: TID, Rich One na Damian Soul
Kwenye picha hiyo juu, TID ameandika: We Back in Bussiness Once Again …Long Live MajaNi,Tanzania Need New Sound Fix this Problem